Wednesday, October 1, 2014

UMUHIMU WA TOBA KWA KANISA LA SASA

Mwl. Elia Agrey
SEHEMU YA PILI

Baada ya kuangalia maana ya TOBA katika ile sehemu ya kwanza kama ambavyo tuliona kuwa TOBA ni kugeuka kutoka katika jambo ambalo Mungu amelikataza na kutenda lile ambalo Mungu ameliagiza kufanya au kutenda.

Katika sura hii nataka tuangalie UMUHIMU wa TOBA kwa kanisa la sasa ambalo ni mimi na wewe uliyepata nafasi ya kusoma somo hili

1.    TOBA INAKUSOGEZA KARIBU NA MUNGU ZAIDI

Toba ya kweli inakusogeza karibu na Mungu na kuyarudisha mahusiano kati ya mtu na Mungu ambayo yaliharibiwa na dhambi.Ule uadui ambao dhambi iliuweka kati yako na Mungu unaondolewa na Mungu anakuwa rafiki yako wa karibu.