![]() |
Mwl. Elia Agrey |
SEHEMU YA PILI
Baada
ya kuangalia maana ya TOBA katika ile sehemu ya kwanza kama ambavyo tuliona
kuwa TOBA ni kugeuka kutoka katika jambo ambalo Mungu amelikataza
na kutenda lile ambalo Mungu ameliagiza kufanya au kutenda.
Katika sura hii nataka tuangalie UMUHIMU wa
TOBA kwa kanisa la sasa ambalo ni mimi na wewe uliyepata nafasi ya kusoma somo
hili
1.
TOBA
INAKUSOGEZA KARIBU NA MUNGU ZAIDI
Toba ya kweli inakusogeza karibu na Mungu na
kuyarudisha mahusiano kati ya mtu na Mungu ambayo yaliharibiwa na dhambi.Ule
uadui ambao dhambi iliuweka kati yako na Mungu unaondolewa na Mungu anakuwa
rafiki yako wa karibu.
“…Warumi
3:23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;..”
Dhambi inafanya Utukufu wa Mungu upungue katika maisha yako
na namna ambavyo Mungu anajidhihirisha kwako kuwa katika kiwango cha
chini.Unaposoma huu mstari unagundua na kujifunza kuwa kama Dhambi inafanya
UTUKUFU wa Mungu kwako kupungua basi TOBA inafanya UTUKUFU wa Mungu kwako kuongezeka
zaidi na zaidi, kwa hiyo unapotubu unamfanya Mungu azidi kujifunua na
kujidhihirisha zaidi katika maisha yako.
Dhambi ambazo zinafanywa na kanisa la
Mungu linamfanya Mungu apunguze udhihirisho wake katika kanisa na vivyo hivyo
dhambi zinazofanywa na Nchi au taifa zinafanya Mungu apunguze udhihirisho wake
katika Taifa. Toba kwa ajili ya Kanisa inamfanya Mungu aongeze udhihirisho wake
katika kanisa lake na Toba kwa ajili ya Nchi inamfanya Mungu aongeze zaid
udhihirisho wake katika nchi.
Angalia kitabu kile cha “…Isaya 57:15 Maana yeye aliye
juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi;
Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na
roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua
mioyo yao waliotubu…”
Sio kila mtu anakaa pamoja na Bwana ingawa wengi wanapenda
kukaa pamoja na Bwana lakini ni wale walio na roho iliyotubu ndio wanaopata
nafasi na fulsa ya kukaa pamoja na Bwana.
Unapotubu kwa roho na kweli Mungu anasema anakusogeza
karibu naye na kukaa pamoja na wewe siku zote.Kwa iyo kanisa linapokuwa na roho
ya toba ndipo Mungu anakaa katikaki yake na ndipo UWEPO wa Mungu unalifunika
kanisa na kulitawala mahali kote na kwa sababu Mungu anakaa milele basi kwa
kupitia TOBA kanisa linakaa pamoja na Mungu milele.
Ukielewa umuhimu wa TOBA unapokuwa umemkosea Mungu wewe
kama kanisa la Mungu hautakaa katika hali ya kuto tubu bali utazitubia dhambi
zako zote maana kwa kupitia TOBA Mungu anakusogeza karibu naye zaidi na zaidi.
Unaposoma katika Biblia unaona watumishi wa Mungu mbali
mbali wakikosea kwa namna moja ama nyingine lakini walipochukua uamuzi wa
kurudi kwa Mungu na kuomba msamaha tunaona Mungu akiwasamehe na kuwasogeza
karibu zaidi na UWEPO wake. Kwa hiyo hata na kwako wewe ni muhimu ukajifunza
namna ya kurudi kwa Mungu kwa njia ya TOBA na ndipo Mungu atakusogeza karibu
zaidi na UWEPO wake.
Damu ya YESU KRISTO ipo ili ikusamehe na kukusafisha zaidi
na kukufanya uwe safi haijalisha ukubwa wa kosa au udogo wa kosa unapo TUBU
Mungu anakusamehe na kukufanya kuwa safi kisha kukusogeza karibu naye.
Hakuna kosa ambalo ni kubwa sana kiasi cha kutosamehewa na
Mungu,Mungu ni Mungu wa msamaha unapotubu na Damu ya YESU ipo kwa ajili ya
makosa ya watu ili kuwasamehe na kuwatakasa kila siku iitwapo leo ili kuwaleta
watu walio safi pasipo na taka yoyote ndani yao mbele za Mungu aliye Mtakatifu.
1
Petro 2:9-10 “…Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu,
watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke
gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi
mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata
rehema, bali sasa mmepata rehema…”
Unaposoma huu mstari unaona Petro anajaribu
kuwaonyesha hawa waliotubu dhambi zao na kumwamini Bwana Yesu katika maisha yao
kitu kilichotokea baada ya wao KUTUBU na kumwamini Kristo anasema ninyi ni mzao
mteule maana yake ni kuwa ninyi sasa ni uzao wa Mungu uliotokana na Mungu
mwenyewe na ni familia ya Mungu mwenyewe na ni watu walio karibu na Mungu na
wanaoishi na kukaa mahali ambapo Mungu yupo.
hivyo unapotubu dhambi zako na kurudi kwa Mungu
wewe unakuwa sio mtu wa kawaida bali mtu wa tofauti unae kaa mahali ambapo
Mungu anakaa. Kwa hiyo tunapotubu kama Kanisa la Mungu,Mungu Baba anazidi
kutusogeza karibu na yeye zaidi nasi tunapata kumjua Mungu zaidi na TABIA ya
Mungu inakuwa TABIA ya KANISA na vitu avipendavyo Mungu ndivyo nasi kama KANISA
tunaanza kuvipenda
Uhusiano uliopotea kati yako na Mungu unarudi
kwa njia ya TOBA pekee.
2. TOBA INAWEKA ULINZI KATIKA
MAISHA YAKO
Jambo
la pili ambalo TOBA inafanya katika maisha ya mtu anae TUBU ni kuweka ulinzi
katika maisha yake.
Ayubu 1:5-10 “…5 Basi ilikuwa, hapo hizo siku za karamu zao zilipokuwa
zimetimia, Ayubu hutuma kwao akawatakasa, kisha akaamka asubuhi na mapema, na
kusongeza sadaka za kuteketezwa kama hesabu yao wote ilivyokuwa; kwani Ayubu
alisema, Yumkini kwamba hawa wanangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu
mioyoni mwao. Ndivyo alivyofanya Ayubu sikuzote.
6 Ilikuwa, siku moja
ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye
akaenda kati yao.
7 Bwana akamwuliza
Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka
katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
8 Kisha Bwana akamwuliza
Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja
aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na
kuepukana na uovu.
9 Ndipo Shetani akamjibu
Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
10 Wewe hukumzingira kwa
ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za
mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi…”
Bwana Yesu apewe sifa!!! Unaposoma katika hii
mistari unaona jinsi ambavyo Mungu na shetani wakizungumza juu ya mtumishi wa
Mungu Ayubu.Shetani alikuwa katika kuzunguka zunguka huku na huko humo ndipo
akakutana na Mungu na Mungu anamuuliza shetani kama amekutana na mtumishi wake
Ayubu
Mstari ule wa tisa na kumi anasema “…
Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote
alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka
katika nchi…”
Mungu hakuanza tu kumzingira Ayubu pande zote
bila sababu pasipo Ayubu kufanya kitu chochote,Ayubu alikuwa na utaratibu wa
kuomba TOBA kwa Mungu kwa ajili yake na kwa ajili ya familia yake,mke wake na
watoto wake na alipokuwa akiomba TOBA kwa ajili yake na familia yake NDIPO
Mungu alijenga UKIGO au UKUTA au WIGO kuwazunguka pande zote kiasi ambacho
shetani hakuona sehemu ya kuingilia kwa Ayubu na kwa familia yake yote aliyokua
anaiombea TOBA kwa Mungu hata pasipo familia yake kujua kuwa inaombewa TOBA.
Jambo la msingi kuelewa ni kuwa unapoomba TOBA
ya kweli kwa Mungu, Mungu anaachilia ulinzi katika maisha yako, hauhitaji
kuomba ulinzi unahitaji kuomba TOBA na Mungu ana kusamhehe na kuachilia ulinzi
wake katika maisha yako.
Adui hawezi kuyagusa maisha yako tena maana
Mungu anakulinda pande zote, kukugusa kwake ni pale ambapo Mungu ameuondoa WIGO
wake kwako kwa kusudi maalumu na kumruhusu shetani akujaribu.
No comments:
Post a Comment