SEHEMU YA KWANZA
![]() |
Mwl: Elia Agrey |
MAANA YA TOBA
Bwana
YESU apewe sifa; ninayo kila sababu ya kumshukuru Mungu anayetupa uzima huu
tulio nao kwa Neema, yaani bure bila kulipia chochote. hivyo basi ni maombi
yangu kwa Mungu kukusaidia kuelewa somo hili ambalo ni muhimu sana kwa kanisa
la sasa kuliko unavyoweza kufikiri na kuyaweka katika matendo yale utakayojifunza.
Fuatana na mimi katika somo hili ili uwe sehemu ya mabadiliko ambayo Mungu
anataka kuyafanya katika Kanisa ambalo ni mimi pamoja na wewe.
Unaposoma
Biblia katika kitabu kile cha Matendo ya Mitume 3:19
Biblia inasema ‘…Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za
kuburudishwa kwa kuwako kwake…”
Katika tafsiri ya the living Bible
Biblia inasema “…Now change your mind and attitude to God
and turn to Him so that He can cleanse away your sins and send you wonderful
times of refreshment from the presence of the Lord…”
Unaposoma katika tafsiri hizi zote mbili za Biblia unapata maana
nzuri ya TOBA ambayo ni kurejea na
kuacha kufanya kitu ambacho ulikuwa unakifanya na Mungu hataki na hapendi wewe
ukifanye.Biblia ya kiingeleza imesema “ Change your mind and attitude ” kwa iyo
unaona kuwa TOBA ni kubadilisha mtazamo wako na mawazo kumulelekea Mungu na
kuacha kuelekea dhambi. Kinachomfanya Mungu akusamehe dhambi zako ni kule
kubadilisha mtazamo wako na mawazo yako yasiyoendana na Mungu. Kwa kifupi
tunaweza kusema kuwa TOBA ni kugeuka
kutoka katika jambo ambalo Mungu amelikataza na kutenda lile ambalo Mungu
ameliagiza kufanya
Si suala tu la kugeuka lakini ni kuenda mbali na yale mambo ambayo
Mungu amekuambia kwa Neno lake ya kuwa usifanye
CHANZO CHA TOBA
Toba imekuja kwa sababu ya dhambi kusingekua na Toba kama hakuna
dhambi na Bilbia inatuambia dhambi ni uasi (1 Yohana 3:4) na uasi ni kuenda
kinyume na maagizo ya Mungu. Kwa iyo kilichosababisha dhambi ije na kutawala
duniani ni uasi ambao mwanadamu aliufanya dhidi ya Mungu.
Dhambi iliingia duniani kwa njia ya KUSIKIA, KUAMINI na KUTII uongo
wa shetani.Adamu ambaye ni mwanadamu wa kwanza na mtangulizi wetu kama baba
yetu wa kwanza ALISIKIA, ALIAMINI, na AKATII uongo wa shetani na ivyo akaruhusu
dhambi kuingia ulimwenguni. Warumi 5:12
“…Kwa
hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti;
na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi…”
Aliyesikia
ni Adamu aliyeamini ni Adamu na aliyetii uongo wa shetani ni Adamu lakini
dhambi ikatufikia watu wote kwa kuwa tu uzao wa Adamu wa kwanza. Unaposikia
unapoamini na unapotii kile ambacho shetani kwa kupitia kitu chochote
amekushawishi kukifanya unatenda dhambi juu ya Mungu na ndipo TOBA inahitajika
katika maisha yako.Mungu hapendi wanadamu waishi chini ya mfumo wa dhambi na
ndio maana alianzisha mfumo mpya kwa mwanadamu wa kumrudia yeye baada ya
kukosea na mfumo huo ni kwa njia ya TOBA. Alimfanya mwanawe Yesu Kristo asiye
na dhambi kuwa dhambi ili kwa kupitia yeye aliye mkamilifu wanadamu wapate
ondoleoo la dhambi milele (1Korintho 5:21)
Kwa hiyo toba iliingia kwa njia ya KUSIKIA, KUAMINI na KUTII kile ambacho Mungu
amesema.Yesu ambaye ni Adamu wa mwisho (1 Korintho 15:45) ALISIKIA, AKAAMINI na
KUTII maagizo ya Mungu na ivyo kuuondoa ule uasi ambao Adamu wa kwanza
aliufanya. hivyo kwako wewe ambaye ni sehemu ya Kanisa la Mungu unapata TOBA
kwa KUSIKIA, KUAMINI na KUTII maagizo ya Mungu katika maisha yako
KWA NINI TUNAHITAJI TOBA
Kuna
mambo mengi ambayo hayaendi sawa katika kanisa la Mungu na ili yaende sawa
tunamuhitaji Mungu aingilie kati kwa njia ya TOBA.Kama Kanisa la Mungu
nikimaanisha mtu aliye mwamini YESU KRISTO likikosea au akikosea mambo mengi
katika maisha yake na ya watu wengine wanaounganishwa naye hayawezi kuenda sawa
hii ikiwa na maana kuanzia katika ngazi ya chini kabisa katika familia na hata
ngazi ya juu zaidi katika taifa hayawezi kuenda sawa maana kuna makosa
yaliyofanywa na hayajatubiwa
Ukisoma
katika kitabu kile cha Warumi 3:23 utaelewa
vizuri kile ninachosema Biblia inasema “… kwa sababu wote wamefanya dhambi, na
kupungukiwa na utukufu wa Mungu;…”
Unapofanya
dhambi yoyote katika maisha yako utukufu na uwepo wa Mungu katika maisha yako
unapungua na hivyo kufanya kiwango cha Mungu kushugulika na maisha yako kupungua
siku hadi siku. Kwa hiyo wewe kama sehemu ya kanisa unapokuwa umefanya dhambi na
haujatubu UTUKUFU na UWEPO wa Mungu uliokuwa katika maisha yako unapungua na hivyo kufanya nguvu na uwepo wa Mungu uliokuwa unashugulika na maisha yako na
wote wanaounganishwa na wewe kupungua katika maisha yako na unapozidi kupungua
ndipo uwepo wa shetani na nguvu za shetani zinapozidi kuyatawala maisha yako na
maisha ya wote uliokuwa unaunganishwa nao kama sehemu ya kanisa
Mahusiano
uliyokuwa nayo na Mungu kama Kanisa yanaharibika kabisa kwa sababu ya
dhambi,Mungu alikuwa rafiki yako lakini anakua adui yako huoni tena sababu ya
kuwa karibu na Mungu unafanya mambo yasiyompendeza Mungu kabisa.Na hiki ndicho
kilichotokea hata kwa Adamu baada ya kumuasi Mungu akaona ajifiche mbali na uso
wa Mungu akijua Mungu hamuoni. Mungu anachohitaji kutoka kwako baada ya kukosea
ni wewe kuomba TOBA kwake na wala sio kujificha mbali naye na kuendelea kufanya
yaliyo maovu zaidi. Sio suala la kuendelea mbele kana kwamba hujui kosa
ulilolifanya na hujali kwamba umefanya bali ni suala la Kurudi na kuzingatia
kisha kuungama dhambi zako ulizozifanya
Ufunuo 2:5”… Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye
matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa
kinara chako katika mahali pake, usipotubu…”
Suluhisho ni
kukumbuka kosa kisha kutubu na kubadilisha muelekeo uliokuwa unaenda nao.Anaposema
kumbuka ni wapi ulikoanguka ukatubu hana maana kwamba uikumbuke dhambi namna
ulivyofanya la hasha ana maana yakumbuke mazingira yaliyokupelekea wewe
ukafanya dhambi kisha epukana na hayo mazingra na ubadilishe muelekeo wako
katika mazingira yaliyokufanya umkosee Mungu. Suala la kuanguka lipo lakini
Biblia inatufundisha kitu kimoja muhimu sana kuwa ukianguka USIKAE hapo hapo na
kukubaliana na hali iyo bali INUKA na UTUBU. Usikae hapo hapo wala usiinuke na
kuendelea mbele KANA KWAMBA hakujatokea kitu bali INUKA na UTUBU
No comments:
Post a Comment