Mwl. ERASTO KIBIKI
Hatima ni lile kusudi la milele ambalo
mwanadamu ameumbiwa alitimize akiwa hapa duniani, kama tunavyosoma katika
biblia kuwa “Daudi baada ya kulitimiza kusudi la Mungu wake akalala na baba
zake”
Hatima {Destiny} ni ule wito unaokufanya uishi hapa duniani na baada ya kuukamilisha unarudi mbinguni kwa Mungu wako.
Hatima ya maisha ni kitu muhimu sana kukijua kabla ya kuvijua vitu vyote, maana hatima ni zile ndoto za maisha yako ambazo kwa hizo unakula, unakunywa, unapata makazi na malazi. Kwa hatima yako unapata pesa inayokuwezesha kuishi vizuri na kuwa msaada katika jamii inayokuzunguka.
Hatima {Destiny} ni ule wito unaokufanya uishi hapa duniani na baada ya kuukamilisha unarudi mbinguni kwa Mungu wako.
Hatima ya maisha ni kitu muhimu sana kukijua kabla ya kuvijua vitu vyote, maana hatima ni zile ndoto za maisha yako ambazo kwa hizo unakula, unakunywa, unapata makazi na malazi. Kwa hatima yako unapata pesa inayokuwezesha kuishi vizuri na kuwa msaada katika jamii inayokuzunguka.
Wengi wamekufa wangali bado wanahitajika hapa
duniani, wamezikwa na ndoto zao zisizotimizika, wamepoteza heshima zao na
maisha yao yaliyokuwa tegemeo kubwa sana duniani kote, kilio chao kinasikika
masikioni mwa wengi, wanajiuliza sana kwa nini watu wema wanakufa mapema kuliko
watu wabaya, maana wabaya wanaishi miaka mingi wakiendelea kutenda uovu.
Si hivyo hii ni vita ya hatima za maisha ya watu, ni mkakati wa shetani na malaika zake wa kuwafanya watu wasiwe msaada kwa jamii zao, kuwabadilishia hatima za maisha ili waishi maisha feki, maana maisha yako ya asili ambayo Mungu amekuumbia uyaishi yametekwa nyara na ndoto zako za maisha zimeibiwa na kufichwa kwenye mapango na mashimo ya kichawi.
Si hivyo hii ni vita ya hatima za maisha ya watu, ni mkakati wa shetani na malaika zake wa kuwafanya watu wasiwe msaada kwa jamii zao, kuwabadilishia hatima za maisha ili waishi maisha feki, maana maisha yako ya asili ambayo Mungu amekuumbia uyaishi yametekwa nyara na ndoto zako za maisha zimeibiwa na kufichwa kwenye mapango na mashimo ya kichawi.
Wewe ulikusudiwa kabisa uwe meneja au mmiliki
wa kampuni yako, uliumbiwa kuwa mwanasheria kabisa ili haki itendeke, uwe
mwalimu ili vijana wapate elimu bora na Mungu atukuzwe kupitia wewe, lakini
umejikuta unaishia kuwa mama ntilie, au mbeba mizigo wa stendi, au mtu
anayeishi maisha yaliyo chini ya kiwango. Hapo hatima yako imetekwa, imeibiwa
na adui amekushinda vitani. Hiyo ni vita lazima upambane kuikomboa kesho yako.
Wengi wanapokutana na magumu ya kimaisha, na
mambo mabaya maishani wanatiana moyo wakisema kuwa “usilie! Jikaze kiume! Maana
maisha ndivyo yalivyo, vumilia!” bila kuchunguza kwa undani chanzo cha tatizo,
hatimaye wanaangukia katika mtego wa ibilisi na kuangamia.
Si kila ugumu wa maisha ndivyo ulivyo au ndivyo unavyotakiwa kuwa! Hapana! Kila kitu kina chanzo chake, inuka ukaishindanie hatima yako, huo ni uonezi na ni mbinu chafu za adui za kukuibia Baraka zako. Uwe hodari na jasiri katika Bwana maana hii ni vita kamili inayopiganwa katika ulimwengu wa roho, jikaze kiume maana bila shaka utashinda, Mungu yuko upande wako; tena walio upande wetu ni wengi kuliko walio katika upande wa adui.
Si kila ugumu wa maisha ndivyo ulivyo au ndivyo unavyotakiwa kuwa! Hapana! Kila kitu kina chanzo chake, inuka ukaishindanie hatima yako, huo ni uonezi na ni mbinu chafu za adui za kukuibia Baraka zako. Uwe hodari na jasiri katika Bwana maana hii ni vita kamili inayopiganwa katika ulimwengu wa roho, jikaze kiume maana bila shaka utashinda, Mungu yuko upande wako; tena walio upande wetu ni wengi kuliko walio katika upande wa adui.
Hatima ya maisha yako [your Destiny] ni
mahali ulipokusudiwa ufike na uishi hapo ili ulitumikie na kulitimiza
shauri/kusudi la muumba wako uliloletwa kwalo na ndilo linalokufanya uishi,
ukiisha kulitumikia shauri hilo hakika yake utalala na baba zako kaburi, yaani
kifo kitakupata nawe hutaonekana tena juu ya uso wa nchi bali utaenda kuishi milele
mbinguni au jehanamu kwa kutegemeana na uhusiano wako na Mungu wako ulipokuwa
hai.
Maisha haya ya kulitumikia na kulitimiza
kusudi uliloumbwa nalo yamefichwa ndani ya muda na nyakati maalum chini ya
mbingu, maana “kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini
ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa; wakati wa kupanda na wakati wa
kung’oa yaliyopandwa. …… Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale
anayojishughulisha nayo?” [Mhubiri 3:1-9] ni muhimu sana kuzijua nyakati na
majira ya maisha yako. Je! Hapo ulipo ndipo kusudi lako la kiuumbaji lilipo?
Je! Ndipo wito wako ulipo? Na je! Huo wito unautimiza ndani ya muda maalum.
Maana hata Gideon aliitwa kwa wakati na
majira yake ili awaokoe waisraeli dhidi ya mateso ya wamidian, na alipotendwa
kwa wakati uliokusudiwa Mungu alimhesabia haki, malkia Esta hakulitambua kusudi
la uwepo wake duniani, yaani hakujua hatima ya maisha yake mpaka pale ndugu
yake Mordekai alipomwambia “… kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo
kutakapowatokea wayahudi msaada wa wokovu kwa njia nyingine, ila wewe
utaangamia pamoja na mlango wa baba yako. Walakini ni nani ajuaye kama wewe
hukuujia ufalme kwa ajili ya wakati kama huo?” [Esta 4:12-17]
Eti! Ndugu yangu ni nani ajuaye kama elimu na
hadhi uliyonayo ni ili uwaletee ndugu zako ukombozi dhidi ya umaskini, ugumu wa
maisha na hali tete ya familia na jamii yako? Yumkini umekuwa kiongozi ili
ulijenge taifa lako katika hali ya kumcha Mungu na kuimarisha maisha ya watu
wako wengi waliokata tamaa ya kuishi. Ni nani ajuaye kama uzuri ulionao ni kwa
ajili ya ufalme wa Mungu na si ukahaba unaoufanya! Ni nani ajuaye kama hatima
yako ipo ili hali njema ya maisha ya watu itokee nawe uwe Baraka kwao.
Adui anafanya vita dhidi yako ili kuziua
ndoto za maisha yako, hakutafuti wewe bali anaitafuta hatima ya maisha yako
popote ulipo. Ndipo sasa unapaswa kujua namna ya kuishindania hatima yako,
umezaliwa ili uwe mshindi siku zote, wewe ni zaidi ya vile ulivyo, usujidharau
kwa vyovyote, umepewa uwezo na mamlaka ipo ndani yako. Kabisa unapaswa kujua
aliye ndani yako ni mkuu kuliko wale wanaokutafuta maishani.
AINA KUU MBILI ZA MAADUI WA HATIMA YAKO
Wapo maadui wakuu wawili wa hatima ya maisha
yako, wanakuwinda usiku na mchana ili kukuangusha na kukupoteza katika uso wa
nchi, maadui hawa kwa asili ni mapacha na wamegawana majukumu ili kukushambulia
ipasavyo nao ni
1.
Adui wa ndani
2.
Adui wa nje
Kiasili hivi ni vyeo tu, yaani kila aina ya
adui ndani yake kuna idara na uongozi mbalimbali unaotenda kazi katika
ulimwengu wa roho. Ni sharti kuwafahamu vizuri na kuzijua mbinu za kuwashinda
na kuwa mshindi kweli kweli.
Adui mbaya zaidi ni Yule wa ndani yako, yeye
anaishi na anatenda kazi kutokea ndani yako, katika fikra na akili zako, katika
moyo wako, katika viungo vyako vya mwili n.k
Adui wa nje anategemea sana msaada kutokea
ndani, yeye amepewa jukumu la kumsadia adui wa ndani na kumuongezea nguvu za
kiutendaji kazi tu.
No comments:
Post a Comment