TAFSIRI
YA MAOMBI
Maombi ni neno lenye
tafsiri mbalimbali na kila mtu hulielezea vile anavyopata ufunuo kwa wakati
huo, upana wake umepelekea watu mbalimbali kuwa na mitazamo tofauti tofauti juu
ya uhalisia wa maombi yenyewe.
Maombi yamejikita
katika nguzo kuu tatu, ambazo ni
1. Muombaji
[mtu/mwanadamu],
2. Muombwaji
[anayeombwa
3. Kipeleka
maombi [mawasiliano]
Maombi yanawasilishwa na pande mbili tofauti zinazotofautiana kiuwezo, ni lazima upande mmoja uwe na nguvu ya kutimiza mahitaji ya upande wa pili, mfano: mwanadamu anapoamua kumuomba Mungu ampe ulinzi wa maisha yake wakati wote au anapoomba rafiki yake amsaidie kifedha, ili kupata majibu ya maombi yake kunahitajika uwezesho wa kimawasiliano baina ya hizi pande mbili.
Maombi yanawasilishwa na pande mbili tofauti zinazotofautiana kiuwezo, ni lazima upande mmoja uwe na nguvu ya kutimiza mahitaji ya upande wa pili, mfano: mwanadamu anapoamua kumuomba Mungu ampe ulinzi wa maisha yake wakati wote au anapoomba rafiki yake amsaidie kifedha, ili kupata majibu ya maombi yake kunahitajika uwezesho wa kimawasiliano baina ya hizi pande mbili.
Ili maombi yaweze kuwa
maombi ni lazima kuwepo na mapatano au makubaliano baina ya hizi pande kuu
mbili zinazotofautiana kwa namna moja ama nyingine kiroho, kimwili, kiuchumi,
kifikra, kielimu, kisiasa, kijamii na kadharika.
Tafsiri
rahisi za maombi ni:-
Maombi ni kuhitaji
msaada katika ulimwengu wa roho ili kutatua mahitaji yaliyopo katika ulimwengu
wa Mwili. Ni ile hali ya kufungua mioyo yetu kwa Mungu ili akutane na mahitaji
yetu, mara zote maombi hayamshushi Mungu chini duniani bali yanaifanya mioyo
yetu inyenyekee na kupata kibali mbale zake.
Maombi ni kumpa Mungu
kibali ama leseni cha kulitimiza kusudi lake kwa kupitia mwanadamu aliyemuumba
hapa duniani, kibali hiki humfanya Mungu apitishe vitu vyake hapa duniani kwa
kupitia mwanadamu.
Maombi ni mawasiliano
yaliyoko kati ya Mungu mtakatifu na mwanadamu aliyeko duniani kwa njia ya Yesu
Kristo na kwa msaada wa Roho mtakatifu.
Kama mawasiliano
yalivyo na umuhumu hapa duniani katika kufanikisha mipango na mikakati ya
kimaisha katika jamii za aina zote, ndivyo maombi yalivyo na umuhimu katika
kuufurahia uhusiaono wetu na Mungu hapa duniani. Ili tuwe na nguvu rohoni na
kuishi maisha ya utakatifu na ya kumpendeza Mungu kila wakati tunatakiwa kuwa
na uhusiano binafsi ulio halisi na baba yetu wa Mbinguni.
Huwezi kumtenganisha
mkristo na maombi, hakuna maombi yasiyokuwa na njia au namna ya kuyawasilisha
na kuyapeleka kwa Yule umuombaye ambaye ni Kristo Yesu kwa kusaidiwa na Roho
Mtakatifu.
Ili mkristo aweze
kuvuta hewa safi na yenye usalama kwa maisha yake yote ya rohoni inampasa awe
na muda wa kutosha wa kuzungumza na Mungu wake kila wakati na kuyatenda yote
anayoagizwa kwa wakati muafaka [hayo ni maombi]
Tumeambiwa kuwa “Tusijisumbue
kwa Neno lolote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushuru,
haja zenu na zijulikane na Mungu (Wafilipi 4:6);
Kwa kusisitiza anasema:-
“Basi kabla ya mambo
yote Mungu anataka dua na sala na maombezi na shukrani, zifanyike kwa ajili ya
watu wote [1 Timotheo 2:1]
Hivyo tuungane pamoja
katika kuliombea kanisa na taifa la Tanzania kwa ujumla.
tushirikishe dondoo za maombi kwa ku comment au kutuandikia maoni kwenye link yetu hapo chini:-
Mungu awe nasi tangu sasa na hata milele, Amina.
No comments:
Post a Comment