KUHUSU SISI

DIRA:
kuwafikia watu wengi kwa kadiri iwezekanavyo kutoka katika makabila yote, lugha zote na mataifa mbalimbali kwa neno la Mungu

DHAMIRA
Dhamira yetu ni kuihubiri injili na kufundisha kweli ya neno la mungu kwa mfumo rahisi na wa kueleweka, ili injili ya Kristo iwafikie mataifa yote kama agizo kuu linavyosema “Enendeni ulimwenguni mwote mkawafanye mataifa kuwa wanafunzi wangu. (Mathayo 28:19-20)

KUANZA KWA HUDUMA
Huduma hii ilanzishwa mwaka 2005 ikiwa na jumla ya washiriki kumi na mbili, wengi wao ni waalimu na wahubiri wa injili, wengine ni waimbaji na waombaji, lengo kuu la huduma hii ni kuliimarisha kanisa yaani mwili wa kristo kwa kuifundisha kweli ya Neno la Mungu kwa usahihi na umahiri mkubwa. Hii ni kutokana na mwili wa kristo hasa makanisani kukosa wahudumu wenye sifa na ujuzi sahihi wa elimu ya Neno la Mungu katika viwango vinavyotakiwa.

MAANA YA JINA
Boanerge ni jina walilopewa Yakobo na Yohana baada ya Yesu Kristo kuwachagua wanafunzi wake kumi na wawili na kuwapa majina (linatoka katika kitabu cha Marko 3:17 “Na Yakobo mwana wa zebedayo na Yohana nduguye yakobo akawapa jina la Boanerge maana yake wana wa Ngurumo”). Kwa kuwa Yeye ndiye aliyewaumba na kuijua asili ya kila kitu akaona hilo jina linawafaa hao yaani BOANERGE ni jina la Kigiriki lenye maana ya WANA WA NGURUMO” ambapo kwa tafsiri ya sasa hili jina linamaanisha wahubiri wa injili wenye moto na nguvu ya Mungu walio jasiri kuihubiri kweli ya Mungu bila kujali hali, mazingira na kipingamizi chochote.

Kutokana na thamani ya hili jina, ndipo neno la huduma likawa ni Mathayo 10:5-8 wenye sifa zifuatazo, pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure. Unao-endana haswa na jina la huduma yaani “WANA WA NGURUMO”

MSINGI WA HUDUMA:
“…. Na katika kuenenda kwenu, hubirini mkisema, ufalme wa mbinguni umekaribia, pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo, mmepata bure, toeni bure.” [Mathayo 10: 5-8]

Neno kuu la huduma ni ile Mathayo 10:5-8, na ukianzia ule mstari wa tano anasema “Hao thenashara Yesu aliwatuma akisema, katika njia ya mataifa msiende, wala katika mji wowote wa samaria msiingie. 6 Afadhari shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli….”

Nyumba ya Israel kwa karne ya sasa ni watu wote walio-okoka ambao wanaitwa mwili wa Kristo, haijalishi upo katika dhehebu gani, maadam umeokoka wewe ni nyumba ya Israel kibiblia. Sasa hao ndio tulioitwa kwao, yaani tuwafundishe kweli ya neno la Mungu, na kuwahubiria ijnili tukisema “ufalme wa mbinguni umekaribia, tupoze wagonjwa, tufufue wafu, tutakase wenye ukoma, tutoe pepo maana tumepata bure ni sharti tutoe bure” [Mathayo 10: 7-8] ndio maana wengi wa wahudumu wa huduma hii ni waalimu na wahubiri, ingawa wapo wengine waimbaji, waombolezaji, wachungaji, wainjilisti na mitume.

Tunahubiri na kufundisha neno la Mungu kwa njia mbalimbali kama mikutano ya hadhara, semina za ndani, makongamano, matamasha, mikesha ya maombi, umisheni na uhamasishaji wa kimaendeleo kwa watu wote. Pia tunatumia machapisho mbalimbali kama vitabu, vipeperushi barua pepe, kwa njia ya mitandao, CD & DVD na kwa mfumo wowote wa ki-electroniki ili injili iyafikie mataifa yote.



No comments:

Post a Comment